Kelvin:
“Bro, jana nilijikuta kwenye
wakati mgumu sana kwa sababu ya ujumbe mmoja tu wa WhatsApp.”
Mimi: “Ujumbe gani?”
Kelvin: “Nilipokea taarifa kwenye group.
Ilisema kuna mabadiliko makubwa yaliyotangazwa na mamlaka fulani. Ujumbe
ulikuwa umeandikwa kwa kujiamini kabisa. Watu wengi walikuwa tayari
wameusambaza.”
Mimi: “Halafu?”
Kelvin: “Bila hata kujiuliza sana,
nikaupeleka kwenye group lingine.”
“Na
kumbe?”
“Baadaye
nikagundua kuwa taarifa ile haikuwa ya kweli.”
Mimi; “Dah! Ulifanya nini?”
“Nilijuta
kwa sababu nilikuwa tayari nimeisaidia kusambaa. Sijui watu wangapi wamesoma
ujume huo bro”
Hapo
ndipo jambo muhimu lilipo.
Changamoto
aliyoipitia Kelvin pia inawapata watumiaji wengine wa mitandao ya kijamii
wanapopokea taarifa.
Kila siku
tunapokea taarifa kupitia WhatsApp, Facebook, TikTok na mitandao mingine.
Baadhi ni za kweli. Baadhi ni za uongo. Nyingine zinaweza kuwa na taarifa ya
kweli lakini zimepotoshwa.
Kwa hiyo
kabla hujabofya Share,
fuata hatua hizi:
1.
SUBIRI
Usisambaze
taarifa mara tu unapopokea. Chukua muda kwanza. Usitake kuoenekana wewe umekua
wa kwanza kupata taarifa na kuisambaza kwenye mitandao ya kijamii.
2.
CHUNGUZA
Jiulize:
- Nani ametoa
taarifa hii?
- Imetolewa lini?
- Chanzo cha awali
ni kipi?
- Kuna ushahidi
gani?
- Taarifa hii
imeandikwa au kuwasilishwa katika muktadha gani?
3.
TAFUTA UTHIBITISHO
Usiegemee
ujumbe mmoja tu. Tafuta taarifa hiyo kwenye vyanzo vingine vinavyoaminika.
Linganisha taarifa kabla ya kuamua kuisambaza.
Kumbuka:
Ujumbe unaweza kuwa umetumwa na rafiki yako unayemwamini. Lakini hiyo haimaanishi taarifa yenyewe ni ya kweli.
Kabla ya Share, jiulize maswali
yafuatayo; Nani amesema? Lini amesema? Chanzo ni kipi? Uthibitisho uko wapi?
Usisambaze taarifa tu. Hakikisha
ni taarifa sahihi.


