Je unatumia Mirungi? Fahamu kuhusu madhara yake kwa binadamu na jamii.

0


#UleviSioDili : Mirungi ni moja ya dawa za kulevya zinazochochea ubongo kufanya kazi kwa kiwango kisicho cha kawaida na mara nyingi huonekana na wengi kama nyongeza ya nguvu au burudani ya muda mfupi, Lakini nyuma ya msisimko huu kuna hatari zinazoshika moyo unaopiga haraka, usingizi unaopotea, migongano na migogoro na hata madhara makubwa kwa afya ya uzazi .

Wataalam wa maswala ya afya wanaeleza kuwa watu wanaotumia mirungi mara kwa mara, hupoteza kidogo kidogo uwezo wa mwili na akili kuendeleza maisha ya kawaida. Vile vile, jamii inayokumbwa na tatizo hili hususani vijana ina hatari ya kupoteza nguvu kazi, amani na ustawi wa kila siku. Kutambua madhara yake ni hatua ya kwanza ya kulinda afya, familia na mustakabali wako.

Kwa mujibu wa shirika la ICCAO Tanzania, Mirungi ni aina ya dawa za kulevya inayochochea mfumo wa fahamu kufanya kazi kuliko kawaida na usababisha mapigo ya moyo na upumuaji kuongezeka. Kemikali zinazoathiri ubongo ni cathinone na  cathine na  mirungi kwa watumiaji au vijana wengi ufahamika kama gomba, miti, gati, mronge, veve, miraa au mbaga.

Kama ulikua unatumia au kama ulikua unapanga kutumia na ulikua ufahamu madhara  ya mirungi, basi fahamu ya kwamba matumizi ya mirungi yana madhara kwa watumiaji ikiwa ni pamoja na;

1. Huongeza shinikizo la damu na kusababisha kiharusi

2. Huathiri mfumo wa uzazi kwa kupunguza nguvu za kiume, ugumba pamoja na utasa

3. Ajali za barabarani kwa wanaotumia vyombo vya moto kutokana na kukosa usingizi

4. Magonjwa ya afya ya akili yanayojitokeza kwa vipindi vya mwezi mchanga

5. Husababisha vidonda kwenye mfumo wa chakula na saratani

6. Kuozesha na kubadilisha rangi ya meno, maumivu ya fizi na harufu mbaya mdomoni

7. Husababisha magonjwa ya ini

8. Hupunguza hamu ya kula

9. Husababisha kukosa choo na kusababisha bawasiri

10. Husababisha uchovu mkali na sonona

11. Husababisha ukatili, fujo, ugonvi na migogoro

12. Husababisha kushuka kwa uzalishaji na kipato.

Elimu hii ya madhara ya madhara ya Mirungi kwa binadamu na jamii inaletwa kwenu na  shirika la ICCAO Tanzania kupitia mradi wa Ulevi Sio Dili kwa kushirikiana na Musoma News Hub


✍️Imeandikwa na Emmanuel Chibasa

     Chanzo: ICCAO Tanzania


#UleviSioDili

#UleviSioDiliVijanaTuamke

#EpukaUleviLindaAfyaYako

#ICCAOTanzania

#MusomaNewsHub

Chapisha Maoni

0 Maoni
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Chapisha Maoni (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top