Jamii Haina Budi Kuachana na Mila na Desturi Zenye Madhara -Neema Ndoboka

0


 

Na WMJJWM-Dodoma

Serikali yaendelea na juhudi za kuchochea Maendeleo katika jamii  kupitia afua mbalimbali ikiwemo  utoaji wa elimu juu  masuala ya mila na desturi zinazozofaa na zile zisizofaa  kupitia mikakati mbalimbali hususani kupitia kushirikiana na wadau wa maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa idara ya Maendeleo ya Jamii Neema Ndoboka alipokua akifungua  kikao cha wadau wanaotekeleza eneo la mila na desturi katika Mpango wa Taifa wa kutokomeza ukatili zidi ya wanawake na watoto(MTAKKUWA) Septemba 17,2025 Mkoani Dodoma.

Neema amewaasa wadau  wa Maendeleo wanaotekeleza eneo hilo kuongeza juhudi zaidi na  kutokukata tamaa kwani  suala la jamii kukubali kuachana mila walizorithishwa vizazi baada ya vizazi si jambo jepesi.

“Serikali inatambua na kuthamini mchango wenu katika kuleta mabadiliko katika jamii lakini suala mila na desturi linachukua muda hivyo mnapaswa kutokukata tamaa na inabidi muendelee kupambana  zaidi kutoa elimu kwa wanajamii na madaliko yatakuja tu” amesema Ndoboka.

Vilevile Ndoboka ametoa wito kwa jamii kukumbatia mila na desturi zinazofaa kwani baadhi ya mila ndiyo asili ya mwafrika na zina umuhimu wake katika kulinda maadili na mienendo ya Jamii. 

“Tunachokipinga ni mila zinazokandamiza na kuumiza baadhi ya makundi katika jamii kwani tunaelewa kwamba kuna mila na desturi ambazo zinazofaa  na zinajenga misingi ya jamii husika  na maadili ya kitanzania”amesema Ndoboka.

Kwa upande Wake Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Carlos Gwamagobe amewaahidi wadau hao wa maendeleo kuwa serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa hali ya juu ili kuweza kufikia malengo yao  ya kuhakikisha mabadiliko chanya yanapatikana katika jamii na Taifa kwa ujumla.

Chanzo: maendeleo ya jamii











Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top