Wadau wa Maendeleo Tanzania Wajadili Ushirikiano wa Kisekta Kujenga Amani Endelevu

0


Wadau kutoka sekta mbalimbali nchini Tanzania wamekutana mtandaoni kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika kujenga amani na mshikamano katika jamii kwa kuzingatia tamko la “Declaration of Peace and Cessation of War (DPCW).”

Kikao hicho cha Tanzania Peace Implementation Committee for the Realization of the SDGs kilichoandaliwa na Heavenly Culture, World Peace, Restoration of Light (HWPL), kilifanyika Agosti 15, 2026 na kuwakutanisha wadau kutoka sekta za sheria za kimataifa, dini, elimu ya amani, vijana, vyombo vya habari na asasi za kiraia.

Joseph Kayinga ni mwandishi wa habari akizungumza katikakikso hicho amesema amani ni msingi wa jamii yenye maelewano na ametoa wito kwa waandishi wa habari kutumia nafasi yao kama jicho na sauti ya jamii katika kuendeleza ajenda ya amani huku pia amesisitiza umuhimu wa elimu ya amani kuingizwa katika mitaala ya shule na vyuo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mapunjo Forum George Cleopa Mapunjo, amesema amani inaweza kuanzia katika familia na kuenea hadi kwenye jamii, taifa na dunia. Amesema amani ya kweli haiwezi kupatikana bila haki na ulinzi wa haki za msingi, huku akieleza dhamira ya kuendelea kushirikiana katika juhudi za kujenga amani kwa kuzingatia misingi ya Ujamaa na kujitegemea.

Naye Zakie Philimon Chatanda kutoka Upendo Media, amesema ushiriki wake katika shughuli mbalimbali za HWPL umemsaidia kuona namna ujumbe wa amani unavyoweza kuwasilishwa na kuenezwa katika jamii na hata kuvuka mipaka ya nchi. Alieleza kuwa ushirikiano huo umeendelea kupanuka hadi katika nchi nyingine kwa lengo la kuchangia ujenzi wa amani katika jamii duniani.

Kikao hicho pia kilihusisha mawasilisho kuhusu uzoefu wa ushirikiano, utangulizi wa madhumuni na misingi ya DPCW, majadiliano ya vikundi na ufafanuzi wa nafasi ya Tanzania Peace Implementation Committee. Washiriki walijadili hatua zinazoweza kuchukuliwa katika jamii ili kuimarisha mshikamano wa kijamii, kujenga mfumo endelevu wa ushirikiano wa amani na kuunganisha juhudi za amani kutoka sekta mbalimbali.








Chapisha Maoni

0 Maoni
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Chapisha Maoni (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top