Na Angela Sebastian
Bukoba : Jeshi la polisi mkoani Kagera limepiga marufuku disco la watoto wakati wa kusherekea sikukuu za Eid na Pasaka ili kuwaepusha na madhara ambayo yamekuwa yakijotokeza siku za nyuma pindi wanapokuwa kwenye kumbi za disco hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari, kamanda wa polisi Mkoa wa Kagera Blasius Chatanda leo ofisini kwakwe amesema jeshi hilo mpaka sasa hawajapaokea taarifa kutoka kwa mtu yoyote ya kuomba kibali ili kuendesha biashara hiyo ya disco toto hivyo, ni marufuku mtu yeyote kufanya hivyo.
Amesema malezi na ulinzi wa mtoto unaanzia nyumbani hivyo amewataka wazazi na walezi kutowaachia watoto kwenda matembezi pake yao siku hizo kwa ajili ya kulinda usalama wao,pia amewataadhalisha watu wote kutoendesha magari wakiwa wamelewa na endapo watabainika kufanya hivyo watachukuliwa hatua kali kwa mijibu wa sheria.


