Kila kizazi kina vita yake.
Kwa vijana wa leo moja ya vita kubwa siyo ukosefu wa fursa pekee, bali ni mtego
wa dawa za kulevya unaonyemelea ndoto zao kimya kimya. Bangi, inayojulikana kwa
majina kama msuba, ganja, blanti, kijiti au ndumu, mara nyingi huonekana kama
kitu cha kawaida au cha kujiburudisha. Lakini nyuma ya moshi wake kuna madhara
makubwa yanayoathiri ubongo, afya ya akili, mahusiano ya kifamilia na hata
mustakabali wa taifa.
Wakati
vijana wakidhani wanatafuta utulivu au kuondoa msongo wa mawazo lakini wataalam
wa afya wanaeleza kuwa bangi hubadilisha
uhalisia, hupunguza uwezo wa kufikiri kwa makini na huweza kufungua mlango wa
matatizo ya kiafya na kijamii yasiyorekebishika kirahisi na madhara mengine ni
pamoja na;
· 1. Huamsha magonjwa ya afya ya akili
· 2. Kikohozi sugu, pumu, vidonda vya koo na
saratani
· 3.Husababisha uraibu
· 4.Hupunguza uwezo wa kufikiri na kukumbuka
· 5.Kuona, kusikia na kuhisi vitu tofauti na
uhalisia
· 6. Kuchochea uhalifu mfano wizi, utapeli na
ukatili
· 7. Kupoteza nguvu kazi ya taifa
· 8. Huvuruga mahusiano ya kifamilia
· 9. Hupunguza ufanisi kazini na mashuleni
· 10. Husababisha matatizo ya uzazi
· 11. Kilimo cha bangi huharibu vyanzo vya maji,
viumbe hai na uoto asilia
· 12. Kukosa mwamko wa maendeleo na kusababisha
umasikini
Elimu hii ya madhara ya bangi kwa binadamu na jamii inaletwa kwenu na shirika la ICCAO Tanzania kupitia mradi wa Ulevi Sio Dili, kwa kushirikiana na Musoma News Hub
Imeandikwa na Emmanuel Chibasa
Chanzo: ICCAO Tanzania
#UleviSioDili
#UleviSioDiliVijanaTuamke
#EpukeniUleviLindaAfyaYako
#ICCAO
Tanzania
#MusomaNewsHub


