Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki Kikao cha kujadili maendeleo ya Utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali (Digital Tanzania Project – DTP) kilichoandaliwa na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, kilichofanyika kuanzia tarehe 16 hadi 18 Februari, 2026 Jijini Arusha ambacho pia kinashirikisha Ujumbe kutoka Benki ya Dunia na wanufaika wa Mradi huo (Project Beneficiaries)
NEMC ni miongoni mwa wadau muhimu katika kufanikisha Utekelezaji wa shughuli za Mradi huo ambapo katika Mradi tajwa NEMC imetekeleza kwa tija na wakati shughuli zote zinazohusiana na Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira.
Aidha, Katika kikao hicho NEMC iliahidi kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi kulingana na taratibu zilizopo.
✍️nemc




