Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa
Watumishi wa Umma (PSSSF) umeanza kutoa pensheni
ya mkupuo ya miezi 36 kwa wategemezi wa wastaafu waliostaafu kwa umri au ugonjwa pekee, hatua ambayo
inalenga kuhakikisha familia za wastaafu zinapata usaidizi wa kifedha baada ya
kifo cha mstaafu.
Kwa mujibu ya taarifa katika jarida
maalum la PSSSF, mfuko huu unatoa huduma mbalimbali za mafao, ikiwemo mafao ya muda mrefu kama vile uzeeni,
ulemavu na mirathi, pamoja na mafao ya
muda mfupi kama vile mafao ya uzazi, ukosefu wa ajira na ugonjwa.
Pensheni ya mkupuo ni huduma mpya iliyoanza kutolewa kuanzia Januari 1, 2025, kwa wastaafu waliostaafu kwa umri au
ugonjwa tu.
Vigezo
vya Kunufaika
Malipo ya pensheni ya mkupuo
yanapatikana kwa wategemezi wa mstaafu
aliyefariki aliyekuwa akilipwa pensheni, na ni kwa mujibu wa Sheria ya Mfuko, Kifungu cha 39 (1) na (2).
Wategemezi wanaostahili ni:
- Mjane au mgane wa mstaafu
- Malipo yanalipwa
kwa wategemezi wa mstaafu wa umri/ugonjwa aliyekuwa akilipwa na pensheni
- Wategemezi
wanaostahili kulipwa ni kwa mujibu ya sheria ya mfuko, kifungu cha 39 (1)
na (2). Mjane/mgane au watoto walio chini ya miaka 18 (miaka 21 ikiwa bado
wapo shuleni
- Malipo kwa
wategemezi yatalipwa kufuatia kifo cha mstaafu aliyefariki dunia kuanzia
tarehe 01, Januari, 2025 au alilipwa mafao kwa kanuni mpya iliyoanza
kutumika tarehe 01,Julai 2022
- Malipo haya
yatakuwa ni sawa na pensheni ya miezi 36 ya mstaafu husika wa umri/ugonjwa
ambaye amefariki
- Pensheni
itakayotumika kulipia pensheni ya Mfuko peke yake iliyokokotolewa kwa
kuzingatia kipindi/vipindi vyake vya utumishi.
- Malipo yote ya
pensheni yaliyolipwa baada ya mstaafu kufariki, yatafidiwa kutoka kwenye
mkupuo wa pensheni ya miezi 36.
- Malipo haya
yatafanyika mara moja kwa kila mstaafu aliyefariki.Mgawanyo wa malipo haya
utafanyika kwa mujibu wa kanuni ya mafao ya PSSSF 17 (2) na (3)
- Malipo haya
yatafanyika kwa pamoja kwenye daftrari la pensheni ya kila mwezi.
Malipo haya yatakuwa sawa na pensheni ya miezi 36 ya mstaafu aliyefariki,
na yatafanyika mara moja kwa kila mstaafu aliyefariki. Mgawanyo wa malipo
utafanyika kwa mujibu wa Kanuni ya
Mafao ya PSSSF 17 (2) na (3), na yataonyeshwa kwenye daftrari la
pensheni ya kila mwezi.
Utendaji
wa Malipo
- Malipo yataombwa kupitia mtandao.
- Msimamizi wa mirathi atatakiwa kufika kwenye ofisi ya mfuko kutoa taarifa
za kifo cha mstaafu na kuwasilisha nyaraka zifuatazo:
- Nakala iliyothibitishwa ya cheti cha kifo cha mstaafu
- Namba ya pensheni au cheki namba ya mstaafu
- Nakala ya fomu ya mahakama ya uteuzi wa usimamizi wa
mirathi
- Kitambulisho cha NIDA au Namba ya Utambulisho wa Taifa
(NIN)
- Baada ya msimamizi kusajiliwa kwenye mfumo wa mfuko, ataweza
kuanzisha dai la malipo kwa
mtandao popote alipo.
- Nyaraka zinazohitajika wakati wa kuanzisha dai ni:
- Fomu maalum ya maombi ya mafao ya mkupuo wa pensheni “Ben.15”
- Nakala iliyothibitishwa ya cheti cha ndoa (ikiwa
marehemu alikuwa ameoa/kuolewa)
- Nakala zilizothibitishwa za vyeti vya kuzaliwa vya
watoto
- Fomu ya “Ben.10”
iliyojazwa kikamilifu na kuthibitishwa na benki/mahakama
- Taarifa za benki za wategemezi
- Mfuko utapokea dai lililotumwa na kulifanyia kazi, huku taarifa zote za maendeleo ya dai zikionekana mtandaoni.
📷Picha
na maelezo kwa hisani ya PSSSF
✍️imeandikwa
na Emmanuel Chibasa



