Simbachawene Awataka Wakazi wa Kagera Kurudi Kuwekeza Nyumbani

0


 Na Angela Sebastian 

Bukoba : Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi George Simbachawene amewataka wanakagera waishio nje ya Kagera  kurudi  nyumbai ili kuwekeza  ikiwa ni kuasisi tamasha la Ijuka Omuka linalowakutanisha wanakagera wote kwa maslai ya vizazi vilivyopo na vijavyo.

Amesema hayo wakati wa kufunga Tamasha la utamaduni la Ijuka Omuka ambapo amewataka wazazi wote nchini kuwafundisha mila,desturi na utamaduni wa wazee wao ili waepuke kujiingiza katika mambo yasiyofaa.

Aidha amewashauri wanakagera kufanya uzalishaji wa tija katika zao la ndizi na bidhaa nyingine  zitokanazo na zao hilo pia kufanya utafiti wa ndizi  zinazofaa kuzalishwa na kuzwpa nje ya nchi  na kuingiza uchumi wa mkoa wa Kageta na Taifa letu

 Kwa upande wa mkuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwassa amesema lengo la Tamasha hilo ni kuirudisha Kagera kwenye uhalisia wake,kujadili maendeleo yao,kuibua fursa zilizopo na kutengeneza mikakati ya kutatua changamoto zinazoukabili wa mkoa huo.







Chapisha Maoni

0 Maoni
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Chapisha Maoni (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top