Wananchi 7,562 wa Kijiji cha Mtukula Kunufaika na Mradi wa Maji Missenyi

0


 Na Angela Sebastian 

Missenyi: Wananchi wa vitongoji nane wapatao 7,562 katika kijiji cha Mutukula Wilayani  Missenyi mkoani Kagera wanatarajiwa kunufaika na mradi wa maji wa kijiji hicho, unaohudumiwa na mamlaka ya Maji safi maji taka na usafi wa Mazingira (BUWASA) ambao umefikia asilimia 70.

Mradi huo  ambao unatagharimu shilingi  Bilioni 1.4  utakapokamilika utaongeza  upatikanaji wa maji katika eneo linalohudimiwa na BUWASA kwa wilaya hiyo kutoka asilimia 86 ya sasa hadi 100.

Kiongzi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2025 Ismail Ali Ussi umetembelea mradi huo na kulidhishwa na maendeleo ya utekelezaji ambapo amesema hayo ni maono ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi hawatembei mwendo mrefu kufuata huduma ya maji .

"Tumelidhishwa na utekelezaji wa mradi huu ambapo unahudumiwa na Buwasa tunawaomba wanachi wa vitongoji vitano ambavyo bado havijapata maji tuwe wavumilivu mradi unakamilika muda si mrefu tunapata maji safi na salama kwasababu nia ya  Dk.Samia ni kumtua mama ndoo kichwani na kuondoa changamoto ya kukosa maji safi na salama"amesema Ussi.

Ameseama ujio wa mwenge wa uhuru katika mradi huo inaashiria kuwa mradi huo utakamilika.kwa wakati maana Mwenge haujawahi kusema uongo.

Mratibu wa Mradi mhandisi Lucas Selebeya meneja Buwasa  wa Wila ya Missenyi, wakati akitoa taarifa kwa Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa juu ya  maendeleo ya mradi amesema mradi ujenzi ulianza Januari 2025  umefikia asilimia 70 ambapo vitongoji vitatu kati ya nane vinapata huduma ya maji safi na salama unatarajiwa kukamilila Desemba 30 mwaka huu na kugharimu shl bil.1.4

Thadeo Kashalala ni mmoja wa wananchi ambao tiyali wameishaunganishiwa  huduma ya maji anasema wanashukuru Serikali kwa kuleta mradi huo, kwani walikuwa wakitumia maji machafu kutoka kwenye madimbwi ambayo wananyweshwa mifugo huku wakati wa kiangazi walitembea kilometa 10 kufuata maji mto Kagera. 







Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top