Mwenge wa Uhuru Wazindua Bweni la Wasichana Katika Shule ya Sekondari Kyaka-Misenyi

0


 Na Angela Sebastian 

Missenyi: Mwenge wa uhuru umezindua bweni la wasichana  wa kidato cha tano na sita lenye vyumba viwili katika shule ya sekondari Kyaka iliyoko Wilayani Missenyi mkoani Kagera.

Bweni hilo ambalo limegharimu shillingi milioni 260 ambapo ni chachu kuwajengea uwezo wanafunzi wa kike  wanaotarajiwa kujiunga na shule hiyo mwaka kesho, kufanya vizuri katika masomo yao,kujiamini na kuepuka adha za kiusalama ambazo watoto wa kike hukumbana nazo wanapotafuta elimu.

Akisoma taarifa ya mradi kwa kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa Ismail Ali Ussi leo,mkuu wa shule hiyo Fadhir Nnko amesema fedha ya ujenzi huo ilitoka Serikali kuu ambapo mradi huo ulianza kutekelezwa Machi 15,2025 na kukamilika Agosti 20 mwaka huu kwa asilimia 100.

"Bweni hilo linaouwezo wa kulaza wanafunzi 160 wa kidato cha tano na sita kwa wakati mmoja ambao wanatarajiwa  kudahiliwa mwaka ujao wa masomo kutoka maeneo mbalimbali ya nchi na itasaidia kuondoa adha za watoto wa kike kutembea umbali mrefu kuja shule na kuepukana na changamoto za kuwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia"amesema Nnko.

Naye kiongozi wa mbio za mwenge Ismail Ali Ussi amesema popote palipojengwa miundombinu bora ya sekta ya elimu lazima watoto wanasomaw

kwaa adilifu,uzalendo na ukamavu wa hari ya juu

"Rais Dk Samia Suluhu Hassan aliona ipo haja leo hii kuwa wapo wanafunzi ambao wanapokaribia kipindi cha mitaihani hutembea kipindi cha masafa marefu kuja kupata huduma hiyo ni kutengeneza uduni wa wanafunzi hao"amesema Ussi 

Amesema uduni huo unatokana na kwamba mwanafunzi anapotembea umbali wa mita 500  kilometa moja au masaa mawili hadi matatu alafu,  arudi nyumbani kwa masaa hayohayo na wakati mwingine anakabiliwa na kipindi cha mitihani kwakweli hapo unakuwa hujatengeneza elimu bora ya mwanafunzi huyo.

"Hapo hujui njiani atakumbana na nini,atakutana na vishawishi gani ambavyo vinamtoa katika suala zima la kupata elimu kwahiyo ndiyo maana  Dk.Samia akaona ipo haja sasa ya kujenga mabweni maalum kama haya ambao ni moja ya shule hizo ili watoto waweze kubaki shuleni na kuepukana na adha hizo"ameeleza Ussi 

Naye mkuu wa Wilaya ya Missenyi kanali mstaafu  Hamis Maige wakati akipokea mwenge wa uhuru kutoka kwa mkuu wa  Wilaya ya Bukoba Erasto Sima amesema mwenge utakagua,utatembelea na kuweka mawe ya msingi Katika miradi saba yenye thamanj ya shilingi bilioni 2.4






Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top