Sio Sahihi Kubeba na Kusafirisha Majumbani Mitungi ya Gesi Kwenye Vyombo vya Usafiri ikiwa Imelazwa -EWURA

0



Na Emmanuel Chibasa

Ni  jambo la kawaida kuona madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda pamoja na vyombo vingine vya usafiri Musoma na maeneo mengine nchini, wakibeba na kusafirisha mitungi ya gesi ya kupikia yenye gesi kutoka kwa watoa huduma na kupelekwa majumbani ikiwa imelazwa.

Hali hii watu wengi wanaweza kuona ni jambo la kawaida kwa kuwa  ni njia rahisi y kwa wateja au watoa huduma kuwafikishia wateja huduma kwa haraka lakini pengine hawana elimu ya madhara na hatari inayoweza kujitokeza.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA)  Inatoa tahadhari kuwa tabia hiyo, inaweza kuwa chanzo cha ajali kubwa ya moto na hata milipuko inayoweza kugharimu maisha ya watu.

Sio jambo geni kuona dereva wa boda boda au baiskeli anaondoka kwenye duka la gesi au barabarani akiwa amefunga mtungi mkubwa wa gesi upande wa nyuma wa pikipiki au baiskeli yake, Mtungi huo umelazwa kwa usawa huku akipita katikati ya magari, waenda kwa miguu na wafanyabiashara wa pembezoni mwa barabara.

.Kwa Nini Mitungi Haipaswi Kulazwa?

Mamlaka ya Udhibiti huduma za Nishati na Maji Kanda ya Ziwa(EWURA),  wanaeleza kuwa mitungi ya gesi ya LPG imeundwa kubebwa na kusafirishwa ikiwa imesimama wima na sio kulazwa kama baadhi ya watu wanavyofanya.

Mhandisi Nyirabu Musira ni Meneja wa EWURA Kanda ya Ziwa anasema sababu ya kusafirisha mitungi hiyo ya gesi ikiwa imesimama ,ni kwamba ndani ya mtungi kuna gesi na kimiminika (liquefied petroleum gas). Mtungi unapolazwa  na kusafirishwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine kimiminika hicho  kinaweza kufika kwenye sehemu ya valve au regulator na kuongeza hatari ya uvujaji wa gesi.

Anasema wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari kwa kusafirisha gesi ikiwa imesimama ili kuepusha uharibifu wa Valve na iwapo uvujaji huo utatokea karibu na moto, sigara, mfumo wa umeme au cheche yoyote unaweza kusababisha mlipuko au moto mkubwa.


Picha ya  Mhandisi Nyirabu Musira akiwaeleza waandishi wa habari mkoa wa Mara madhara ya kubeba na kusafirisha mitungi ya gesi majumbani ikiwa imelazwa

‘Unapokua unatumia gesi hakikisha eneo gesi ilipo kuna hewa ya kutosha na madirisha yako wazi, na endapo utahisi harufu ya gesi ujue gesi yako inavuja hivyo unatakiwa uchukue tahadhari kubwa kwa mfano utakiwi kuwasha moto au kuwasha na kuzima swichi ya umeme kukiwa na hali hiyo, sababu swichi ya umeme unapowasha au kuzima wakati gesi inavuja inaweza kusababisha mlipuko” Amesema Nyirabu

Kadiri matumizi ya gesi ya kupikia yanavyozidi kuongezeka nchini, wataalamu wanaonya kuwa usalama wa usafirishaji wa mitungi unapaswa kupewa uzito sawa na usalama wa matumizi yake majumbani. Bila elimu na ufuatiliaji wa kutosha, mitungi ya gesi inayobebwa na kusafirishwa majumbani  ikiwa imelazwa kwenye boda boda na vyombo vingine vya usafiri inaweza kuleta madhara

Chapisha Maoni

0 Maoni
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Chapisha Maoni (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top