Naibu Meya ambae ni Diwani wa kata ya Nyasho katika Manispaa ya Musoma Haji Mtete amewataka watumishi wa serikali za Mitaa na kata, kusimamaia majukumu yao vizuri Kwa mujibu wa Sheria kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarishwa katani humo.
Kauli hiyo ameitoa Leo kwenye kikao Cha WDC Cha robo ya pili ya mwaka 2025/2026kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kata hiyo uliopo ofisini hapo
Mtete amesema mipango ambayo inahitaji kufanyiwa kazi Kwa haraka yafanyiwe haraka ili kutatua changamoto Kwa lengo kupata mafanikio mazuri.
Kuhusu elimu amewataka walimu wakuu kuwapa taarifa wazazi juu ya masuala ya majukumu ya shule badala ya kuwaeleza watoto Kwa kuwa wao hawahusiki na majukumu ya shule .
Aidha amewataka kuwashauri wazazi kuwafanyia vipimo vilivyo sahihi watoto wao pindi wanapowapeleka watoto wao kuanzia kidato cha kwanza ili kujua hali za afya zao kunusuru changamoto za afya shuleni badala kutoa taarifa zisizo sahihi.
"Nendeni mkatoe elimu juu ya suala hili la vipimo Kwa jamii na wazazi Ili kusaidia watoto pindi wanapokuwa shuleni maana itasaidia kuelewa afya zao Kwa usahihi."amesema Naibu Meya Mtete.
Licha ya hilo,pia eneo la machinjio ya kuku limeguswa kuwa sio eneo rafiki kimazingira na kuwataka kuchukua hatua za kisheria na kwamba wafanyabiashara kwenye maeneo ya maduka waweke dazibini za taka badala ya kutupa ovyo takataka.
Katika idara ya Kilimo,ufugaji na uvuvi,amemuagiza Afisa mifugo kuchukua Sheria dhidi ya wafugaji wanahifadhi mifugo yao kutosababisha mgogoro ya uharibifu wa mazao kwa wakulima .
Kwa upande wake mtendaji wa kata hiyo RaymundMwambujule amewashauri watendaji wenzake wa Mitaa kwenda kusimamaia vizuri vitendo viharifu vinavyofanywa Mitaa I badala ya kuwaachia venyeviti na Askari Kwa kuwa serikali imewapa dhamana hiyo .



