Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekutana na muwakilishi wa ujumbe wa Umoja wa nchi za Ulaya (EU) nchini Tanzania na kujadili namna Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii zinavyofanyika kwa Tanzania na jinsi wanavyoweza kushirikiana na Baraza hususani katika masuala ya kimazingira kwa upande wa Sekta ya madini hasa madini muhimu (Critical Minerals)
Kikao hiki kilijadili miongozo iliyopo na kuainisha maeneo yanayohitaji usaidizi wao ili kuwezesha uzingatiaji wa Sheria kwa miradi ya madini inayowekezwa nchini.
Chanzo: NEMC


