Wananchi Kata ya Mabira - Kyerwa Waipongeza Serikali kwa Kuanza Ujenzi wa Barabara kwa Kiwango cha Lami

0


Na Angela Sebastian 

Kyerwa: Wananchi wa kata Mabira Wilayani  Kyerwa wameipongeza serikali  kwa kuanza ujenzi wa  Barabara ya Nkwenda - Mabira  kwa kiwango Cha Lami  ambapo wamesema kuwa mradi huo  ukikamilika  wataongeza wateja  wa kununua  mazao yao na kurahisisha usafirishaji wa mazao.

Ramadhan Robert na Bosco Gabriel wakazi wa Mabila wamesema wamekuwa wakikutana na Athari za vumbi na  mali zao kuchafuka hali inayosababisha  kukosa soko  hasa mazao yakijaa vumbi,ujio wa mradi huo kama wafanyabiashara umewapa matumaini ya kuuza bidhaa zao zikiwa safi.

Meneja wa TARURA wilaya ya Kyerwa Yezron mbasha amesema kuwa mradi huo umegharimu kiasi Cha shilingi Milioni 471.3 ikiwa ni fedha ya Serikali inayotokana na Tozo za Mafuta.

Amesema kukamilika kwa Mradi huo kutaongeza Adhi ya mji wa mabira na Kusaidia usafirishaji wa mazao kutoka katika eneo hilo hadi maeneo mengine ya wilaya hiyo na wilaya jirani.

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ismail Ussi amewataka wananchi kutunza na kulinda Miradi hiyo huku akiipongeza TARURA kwa kutekeleza miradi yenye Viwango  na yenye ubora ikiwa ni pamoja kuongeza kasi ya upatikanaji wa Barabara za lami katika vijiji na maeneo yanayokua kwa Kasi.




Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top