Waliohama Chadema: Wanakwenda kukifufua Chaumma

0

 Kuna wimbi la wanasiasa na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kukihama chama hicho kikuu cha upinzani na kuhamia chama kingine cha upinzani cha Ukombozi wa Umma (Chaumma).


Mei 19, 2025, Mwenyekiti wa Chaumma, Hashim Rungwe aliwapokea baadhi ya vigogo hao; akiwemo Salum Mwalim ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chaumma, Devotha Minja, Makamu Mwenyekiti Bara na Benson Kigaila, Naibu katibu Mkuu Bara.

Taarifa za vyombo vya habari vya ndani nchini Tanzania zinaeleza, mamia ya wafuasi wengine wa Chadema wako njiani kuhamia Chaumma. Bila shaka hizi ni taarifa za neema kwa chama hicho na taarifa mbaya kwa Chadema.

Mwanasiasa wa ngazi ya juu anapohama chama kimoja kwenda kingine, kuna mambo mawili ya kuyatazama. Je, mafanikio yake ya kisiasa yatakibeba chama anachohamia au mafanikio ya chama hicho yatambeba yeye? Twende polepole, utaelewa.

Katika kesi hii ya vigogo hawa wa zamani wa Chadema – ambao wote watatu wamepata kuwa katika nafasi za juu za uongozi katika chama hicho, inaonekana kwa hakika mafanikio yao kisiasa ni makubwa, kuliko mafanikio ya Chaumma.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top