Na Angela Sebastian
Bukoba: Jeshi la Polisi mkoani Kagera limetoa onyo kwa wananchi mkoani humo na kuwataka kufuata sheria baada ya kupiga kura Oktoba 29 mwaka huu kuondoka kwenye vituo vya kupigia kura na kurudi nyumbani.
Amesema hayo leo, wakati akiongea na waandishi wa habari mjini Bukoba, kwamba zimebaki siku tano pekee kufanyika uchaguzi wa Rais,wabunge na madiwani.
Amesema kuwa,zipo taarifa zinazoenezwa kwamba kutakuwa na ulindaji wa kura utakaofanywa na baadhi ya wananchi na kwamba jukumu hilo linafanywa na jeshi la polisi sio wananchi.


