Khaldi Nsekela Amshukuru Dkt. Samia Kutoa Fedha za Maendeleo - Kyerwa

0


 Na Angela Sebastian 

Karagwe : Mgombea ubunge wa jimbo la Kyerwa kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM) Khaldi Mussa Nsekela amemshukuru Dk. Samia Suluhu Hassan

 kwa kutoa shilingi  bilioni 84 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo Wilayani Kyerwa tangu alipoingia madarakani.

Nsekela ametoa shukrani hizo leo katika mkutano mkubwa wa kunadi Ilani ya CCM na kuomba kura za mgombea Urais Dk.Samia Suluhu  Hassan uliofanyika uwanja wa Kayanga Wilayani Karagwe.

Amesema Dk.Samia hana deni kwa wana Kyerwa bali wao ndio wanapaswa kulipa shukrani kwa kumpigia kura nyingi ifikapo Oktoba 29 mwaka huu.

"Wanakyerwa wanasema wanasubiri wakati ufike wakupigie kura za kutosha kutokana  na sababu zifuatazo ambazo ni pamoja na kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo miundombinu ya Elimu,Afya,maji na Umeme ambayo imegharimu sh.bil 84 na kupanda kwa bei ya zao la kahawa kutoka sh.1000 hadi  8000 kwa kilo"anasema Nsekela 

Anasema Ilani ya CCM imesheheni mambo mengi mazuri yanayomgusa kila mwananchi hivyo wanakyerwa wana imani  Dk Samia anaendelea kutekeleza yote aliyoyaaahidi ili wananchi wake waendelee kunufaika na matunda ya nchi yao.










Chapisha Maoni

0 Maoni
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Chapisha Maoni (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top