Taasisi Tatu za Haki Jinai Zatakiwa Kurekebisha Kasoro Zinazoathiri Utendaji Haki

0


 Na. Innocent Kansha na Arapha Rusheke - Dodoma

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju, amefungua kikao kazi cha menejimenti na viongozi wa mikoa na wilaya kutoka Taasisi za Haki Jinai zinazounda Utatu katika Ukumbi wa Kituo cha Jakaya Kikwete Convention, Jijini Dodoma Agosti 19, 2025.

Akizungumza na washiriki, Jaji Mkuu Masaju alisisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa mshikamano na kwa uzito unaostahili akibainisha kwamba; haki ni msingi wa amani, maendeleo na ustawi wa Taifa.

“Tunapojihusisha na masuala ya haki, tunapaswa kulichukulia jukumu hilo kwa uzito, kwani haki ni msingi wa maisha ya pamoja na haki hupendwa na Mwenyezi Mungu. Huu ni mkutano wa muhimu ambao umenisukuma na mimi kuja. Nimeona kaulimbiu zenu ambazo ni za msingi sana. Nikianza na Mahakama ambao ni waalikwa, sisi tuna kanuni za uendeshaji wa ofisi ambazo ndiyo misingi mikuu inayotengeneza kaulimbiu na salamu kama ambavyo tumeziona hapa,” alisema Jaji Mkuu Masaju.

Mhe. Masaju aliongeza kuwa, Mahakama wao wana kitu kinaitwa weledi, uadilifu na uwajibikaji, ‘ukiangalia hiyo misingi (core values) ya ofisi zenu inaleta imani kwamba, mmedhamiria kwa dhati kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi ipasavyo ili kudumisha amani na usalama wa Taifa,’ alisema.

Jaji Mkuu alisisitiza Sekta ya Sheria kuhakikisha inatenda haki kwani kwenye Dira ya Mahakama kuna kaulimbiu ambayo inasema haki sawa kwa wote ambayo ipo katika ibara ya ‘107A sub article 2 a na d ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inasema ‘kutenda haki sawa kwa wote mapema ipasavyo’ huku a na b ikisema, ‘kutenda haki kwa wote bila kujali hali ya mtu kijamii au kiuchumi’ na ‘kutochelewesha haki bila sababu ya kimsingi.’

@mahakama ya tanzania







Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top