Elimu: Fahamu Kanuni za Ubora wa Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira na Fidia Kwa Mteja Endapo Umekatiwa Maji Kimakosa

0


#UKATAJI  WA  MAJI

Kanuni za ubora wa huduma za Maji na Usafi wa Mazingira( Ubora wa Huduma na Leseni za Mwaka 2020; Tangazo la serikali Na: 849, Viwango vya ubora wa huduma pamoja na gharama za fidia kwa kushindwa kufikia viwango vilivyowekwa. Kanuni ya 34(3) inazitaka mamlaka za maji zilizopewa leseni kufikia viwango vya kutoa huduma zitakazowajibika kulipa fidia kwa waathirika.

Kanuni za ubora wa huduma za maji na usafi wa Mazingira inaeleza kuwa endapo mteja amekatiwa huduma ya maji kimakosa itatakiwa ndani ya masaa 24 huduma kurejeshwa baada ya taarifa kutolewa  na endapo mtoa huduma atashindwa kufikia viwango vilivyowekwa mtoa huduma atamlipa mteja shilingi 100,000.00 fidia ya msingi na shilingi 5,000 kwa kila siku inayoongezeka bila tatizo kutatuliwa.

Imeandikwa na Emmanuel Chibasa

Chanzo: ewura ccc

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top