Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) yazindua rasmi mradi wa MWANAMKE THABITI wenye lengo la kutokomeza aina zote za ukatili na ubaguzi dhidi ya wanawake kwa kuhimiza mabadiliko ya kisheria na kuwawezesha wanawake hususan walioko maeneo ya pembezoni kujitambua, kujitetea na kukabiliana na ukatili kuanzia ngazi ya familia hadi katika jamii.
Mradi huu umezinduliwa na mgeni rasmi, Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bi. Vickness Mayao, aliyeunga mkono juhudi zetu za kuleta usawa na haki kwa wanawake wote wa Tanzania.
#TAWLAat35
#MwanamkeThabiti
#HakiHainaJinsia