Na Angela Sebastian- Kyerwa
Msofe amesema kuwa serikali imeanzisha zoezi hilo ili kuwatambua wenyeji na wageni wanaishi katika Wilaya hiyo kwa utaratibu maalumu ikiwa na lengo la kulinda usalama wa Wilaya hiyo na wananchi wake.
Msofe ametoa agizo hilo leo katika kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo ambacho kimejadili taarifa ya utekelezaji ya miradi ya maendeleo kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/2026 ambapo,amesema uandikishaji huo ni nguzo muhimu ya kuimarisha ulinzi na usalama wa Wilaya hiyo na nchi kwasababu Wilaya hiyo iko mpakani.
Wakati huohuo baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo wametoa wiki moja kwa wazazi wote ambao hawajapeleka watoto wao waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza kuripoti shuleni kuhakikisha wanawapeleka shule hata kama hawana sare za shule uku wakisema kuwa baada ya wiki moja msako mkubwa wa kuwakamata wazazi hao utaaanza rasmi na hatua kali za kisheria zitachukuliwa .










